Skip to content

Makala

Macron auona upande wa pili wa shilingi barani Afrika

  • Makala

WAKATI Ufaransa ikiendelea kupoteza kambi zake kadhaa za kijeshi barani Afrika, raiswa nchi hiyo, Emmanuel Macron, katika safari ya kimyakimya kwenye kituo cha mwishocha operesheni za nchi hiyo huko Djibouti, amekiri kwamba Afrika inapitia kwenyemabadiliko. Kwa mujibu wa rais huyo sababu kuwepo kwa mabadiko aliyoyashuhidia barani Afrika ni kutokana na maoni ya umma na serikali za nchi hizo na kueleza kuwa nafasi ya Ufaransa banihumo nayo lazima ibadilike. Katika safari hiyo, Macron amekiri kwamba kambi ya kijeshi ya Ufaransa nchini Djibouti inaweza kuwa na nafasi muhimu zaidi na kukiri kuwa Ufaransa inalazimika kubadilishamtazamo wake wa zamani dhidi ya uwepo wa majeshi yake barani Afrika. Macron pia ametangaza kuwa majukumu ya kambi ya kijeshi ya Ufaransa huko Djibouti yataangaliwa upya na kusema kambi hiyo inapaswa kutumika kama sehemu ya utumiaji nguvukatika baadhi ya misheni za Ufaransa barani Afrika.… Read More »Macron auona upande wa pili wa shilingi barani Afrika

Upatu: Mbinu yakujikwamua yenye tamu na chungu

  • Makala

NA MWANDISHI WETU KUCHEZA upatu imekuwa ni mtindo ambao wanawake wengi wamekuwa wakitumiakama njia ya ya kujikwamua kupata fedha au mtaji kwaajili ya kuendesha shughulimbalimbali za maisha yao ya kila siku.  Wanawake saba katika kundi la wanawake 10 waliofanya mahojiano na makala haya wamewahikushiriki katika aina mbalimbali za upatu.  Hata hivyo mtindo huo umekua ni fursa yenye tamu na chungu inayowakabili wanawake wengikutokana na changamoto za mfumo wa uendeshaji wake.  Upatu upo aina mbalimbali kulingana na mfumo wa uendeshaji wake, kwa mfano upatu wa hisaambao ambao kundi la wanawake wanaungana katika kuweka kiasi kidogo kupata fursa ya kukopa kiwango maalumu bila riba ya marejesho. Pia kuna aina ya upatu unaohusisha vikundi vya ushirika, upatu wa vikundi vidogo vya uwekajina ukopaji kwa riba ambao maarufu mitaani kama (kausha damu), na nyengine.  Upatu unafanyika katika maeneo ya kazi mfano maofisini, majirani, na hata kwa wanafamilia.  Mtindo uliozoelekea zaidi upatu ni wa vikundi vidogo vya wasichana na wanawake katika maeneo ya makazi ambao wanaungana na kuweka utaratibu wa kuchangiana kiwango maalumucha pesa ambacho kila mshiriki atalamizika kutachangia kila baada ya muda.  Vikundi hivi ambavyo mara nyingi inakuwa ni majirani, marafiki au familia vinakuwa na kiongozi maalumu anaechaguliwa miongoni mwa wanakikundi maarufu kama “kijumbe”.… Read More »Upatu: Mbinu yakujikwamua yenye tamu na chungu

Urusi inatumia ‘warembo’ kufanya ujasusi Marekani

  • Makala

MATAIFA mbalimbali ulimwenguni yanatumia mbinu kadhaa za kijasusi katika kuhakikisha yanadhibiti viasharia vya uvunjifu wa amani na kuimarika kwa usalama wa mataifa hayo. Katika mataifa kadhaa wanawake kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakitumiwa kwenye shughuliza kijasusi na kiukweli wamekuwa na mafanikio mazuri katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Urusi katika kuhakikisha linapata taarifa za kijasusi kutoka kwa hasimu wake taifa la Marekani, liliandaa wanawake warembo wenye kuvutia na kuwatumia kwa ajili ya kazi ya kijasusi. Tabasamu za warembo hao zilikuwa za kuvutia, urembo wao ulikuwa kama chambo na mishenizao katika kuhakikisha wanafanikiwa katika majukumu yao zilikuwa za siri kubwa. Warembo wao walijenga mahusiano ya karibu na wanaume mbali mbali nchini Marekani, ambapo lengo ni moja tu nalo ni kukusanya habari muhimu kuhusu mipango ya siri na mikubwaya serikali ya Marekani na kuhakikisha kwamba Urusi ilifahamu yote yaliokuwa yakiendeleanchini humo. Wengi waliishi nchini Marekani kwa miaka na hata kuolewa na kuanzisha familia nchini humo. Katika usiri wa maisha yao uliojaa mengi ambayo yalikuwa ni kwa manufaa kwa Moscow. Baadhi ya warembo waliopewa mafunzo ya kijasusi kuisaidia Urusi kufahamu yote yaliyokuwayakifanyika ndani na nje ya serikali ya Marekani na washirika wake. Kwa miaka mingi ilishukiwa kwamba Urusi haikuwa imekomesha oparesheni zake… Read More »Urusi inatumia ‘warembo’ kufanya ujasusi Marekani

Pages: 1 2 3